Mkurugenzi aondoa sintofahamu kuhusu Sumbawanga mpya


Mkurugenzi wa Mnaispaa ya Sumbawanga Jacob Mtalitinya ameondoa sintofahamu iliyokuwa imesambaa katika manispaa hiyo juu ya maagizo na maelekezo mablimbali aliyoyatoa katika kuboresha huduma kwa kukusanya mapato na kumsaidia mwananchi mmoja mmoja kujiboreshea maisha katika manispaa hiyo.

Mtalitinya alisema kuwa sula la vibali vya ujenzi na leseni za makazi imetafsirika tofauti lakini azma ni kuipima Manispaa kwa asilimia 100 na kuwa huo ni mwendo wa kufanya upimaji.

Tangu kuwasili kwa Mkurugenzi huyo mapema mwezi wa nane mwaka huu wananchi wengi wamekuwa wakipotosha maelekezo anayoyatoa na matokeo yake kueleweka vibaya kwa wananchi wengi wa Manispaa ya Sumbawanga.

 “Unapotaka kujenga jengo lako, unashauriwa kuepuka usumbufu, upate kibali kutoka ofis ya Mkurugenzi na utaratibu wa jengo utakaolifanya, tumeweka nguvu sana kwenye kata za mjini lakini haimaanishi hata kata hizi za pembezoni hazitakiwi kutii sheria hiyo. Leseni ya makazi tunakusudia kuipima Manispaa yetu kwa asilimia 100,” Alibainisha.
Mkurugenzi wa Mnaispaa ya Sumbawanga Jacob Mtalitinya

Pia alizitaja faida za leseni ya makazi ikiwa ni pamoja na kuwa mmiliki halali wa eneo, kurasimisha makazi ili kupata huduma za msingi kama vituo vya afya, barabara na maeneo ya wazi pamojanna kupata hatimiliki itakayodumu kuanzia mika 33 hadi 99.

Ameyasema hayo katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika soko la Kaswepepe, kata ya Sumbawanga Asilia, Wilayani Sumbawanga jambo ambalo lilipendezwa na wananchi waliohudhuria katika mkutano huo na hatimae kuelewa lengo la Mkurugenzi.

Mmoja wa wananchi waliohudhuria Ditmali Mwageni alisema kuwa walishangazwa na kitendo cha mkurugenzi huyo kuwaamuru watu kupaka rangi mabati kulingana na maagizo ya kila kata kuwa na rangi yake, lakini kwa ufafanuzi alioutoa nadhani ameeleweka vyema na wananchi waliohudhuria.

“Kusema kwake kuwa agizo hilo linawahusu wale tu ambao wanaanza kujenga sasa, hapo tumeelewa kuliko tulivyokuwa tunasikia kwamba watu wote wapake rangi za mabati kulingana na rangi ya kila kata, kwakuwa tu ni agizo la mkurugenzi, hiyo haikuwa sawa, nyumba zenyewe za zamani, mabati yamechoka, utekelezaji wake ungekuwa mgumu, lakini kama katoa miaka mitano Kwetu basi sawa,” Alisema.

Miongoni mwa masuala yaliyozua mzozo ni agizo la kila kata kuwa na rangi yake ya bati, kupata kibali cha ujenzi kabla ya kuanza ujenzi, kuwa na leseni ya makazi pamoja na mazoezi mbali mbali ya upimaji yanayoendelea katika manispaa hiyo.


Comments