Mkurugenzi wa Mnaispaa ya Sumbawanga Jacob Mtalitinya
ameondoa sintofahamu iliyokuwa imesambaa katika manispaa hiyo juu ya maagizo na
maelekezo mablimbali aliyoyatoa katika kuboresha huduma kwa kukusanya mapato na
kumsaidia mwananchi mmoja mmoja kujiboreshea maisha katika manispaa hiyo.
Mtalitinya alisema kuwa sula la vibali vya ujenzi na
leseni za makazi imetafsirika tofauti lakini azma ni kuipima Manispaa kwa
asilimia 100 na kuwa huo ni mwendo wa kufanya upimaji.
Tangu kuwasili kwa Mkurugenzi huyo mapema mwezi wa nane
mwaka huu wananchi wengi wamekuwa wakipotosha maelekezo anayoyatoa na matokeo
yake kueleweka vibaya kwa wananchi wengi wa Manispaa ya Sumbawanga.
“Unapotaka
kujenga jengo lako, unashauriwa kuepuka usumbufu, upate kibali kutoka ofis ya
Mkurugenzi na utaratibu wa jengo utakaolifanya, tumeweka nguvu sana kwenye kata
za mjini lakini haimaanishi hata kata hizi za pembezoni hazitakiwi kutii sheria
hiyo. Leseni ya makazi tunakusudia kuipima Manispaa yetu kwa asilimia 100,”
Alibainisha.
Mkurugenzi wa Mnaispaa ya Sumbawanga Jacob Mtalitinya |
Pia alizitaja faida za leseni ya makazi ikiwa ni pamoja
na kuwa mmiliki halali wa eneo, kurasimisha makazi ili kupata huduma za msingi
kama vituo vya afya, barabara na maeneo ya wazi pamojanna kupata hatimiliki
itakayodumu kuanzia mika 33 hadi 99.
Ameyasema hayo katika mkutano wa hadhara uliofanyika
katika soko la Kaswepepe, kata ya Sumbawanga Asilia, Wilayani Sumbawanga jambo
ambalo lilipendezwa na wananchi waliohudhuria katika mkutano huo na hatimae
kuelewa lengo la Mkurugenzi.
Mmoja wa wananchi waliohudhuria Ditmali Mwageni alisema
kuwa walishangazwa na kitendo cha mkurugenzi huyo kuwaamuru watu kupaka rangi
mabati kulingana na maagizo ya kila kata kuwa na rangi yake, lakini kwa
ufafanuzi alioutoa nadhani ameeleweka vyema na wananchi waliohudhuria.
“Kusema kwake kuwa agizo hilo linawahusu wale tu ambao
wanaanza kujenga sasa, hapo tumeelewa kuliko tulivyokuwa tunasikia kwamba watu
wote wapake rangi za mabati kulingana na rangi ya kila kata, kwakuwa tu ni
agizo la mkurugenzi, hiyo haikuwa sawa, nyumba zenyewe za zamani, mabati yamechoka,
utekelezaji wake ungekuwa mgumu, lakini kama katoa miaka mitano Kwetu basi
sawa,” Alisema.
Miongoni mwa masuala yaliyozua mzozo ni agizo la kila
kata kuwa na rangi yake ya bati, kupata kibali cha ujenzi kabla ya kuanza
ujenzi, kuwa na leseni ya makazi pamoja na mazoezi mbali mbali ya upimaji
yanayoendelea katika manispaa hiyo.
Comments
Post a Comment