PS 3 YABORESHA SEKTA YA AFYA NCHINI

WAKATI Serikali inatarajia kuajiri katika sekta ya afya watumishi wapya 7680 (6180 wa Ofisi ya Tamisemi na 1500 wa Wizara ya afya), halmashauri nchini zimetakiwa kutumia ripoti za mfumo wa WISN plus POA iliyorahisishwa kusambaza watumishi wapya kwa kuzingatia uzito wa kazi na mahitaji kama yalivyoainishwa kwenye taarifa hizo.
Mshauri wa rasilimali watu kutoka Mradi wa Uimarishaji wa Mifumo ya Sekta za Umma PS3, Zawadi Dakika, akitoa maelekezo  kwa  Zuberi Mshamu afisa rasilimali watu halmashauri ya wilaya ya tunduru mkoani Ruvuma katika  mafunzo ya kuwajengea uwezo maafisa utumishi na wataalamu wa afya wa halmashauri za mkoa wa Ruvuma juu ya namna bora ya upangaji wa watumishi katika vituo vya kutolea huduma kwa kuzingatia mahitaji. Mafunzo hayo ya siku mbili yanafanyika mkoani Mtwara yakiendeshwa na mradi wa PS3 kwa ufadhili wa shirika la misaada la marekani la USAID.

Kauli hiyo imetolewa katika kikao kazi kilicholenga kuwasilisha matokeo ya uchambuzi wa mahitaji ya watumishi kwa kutumia mfumo wa WISN plus POA iliyorahisishwa kinachofanyika mkoani hapa.
Mfumo wa WISN plus POA hutumika kukokotoa mahitaji ya watumishi kwa kila kada katika vituo vya kutolea huduma kwa kuzingatia uzito wa kazi katika kituo husika.
Kwa sasa mfumo huu unatumika kwa ajili ya vituo vya afya na Zahanati tu, ukijumuisha kada mbalimbali zilizopo katika ngazi hizo za utoaji huduma ambazo ni waganga (MO), waganga wasaidizi (AMO), tabibu (CO), tabibu wasaidizi (CA), maafisa wauguzi (NO), maafisa wauguzi wasaidizi (ANO), na wauguzi (EN).
Kikao kazi hicho pia kilitumika kuzijengea uwezo Halmashauri na Mikoa ili ziweze kutumia WISN plus POA iliyorahisishwa kusambaza watumishi wapya, na katika kuomba watumishi wapya.
Akizungumza katika kikao kazi hicho  kilicholenga kuwasilisha matokeo ya zoezi la kubaini mahitaji ya watumishi kwa kutumia mfumo wa WISN PLUS POA iliyorahishwa Mganga Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam  alisema  mfumo huo ni toleo jipya unaowezesha kutumia taarifa kutoka mfumo wa DHIS 2 kwa ajili ya kukokotoa mahitaji ya watumishi, hivyo kupunguza gharama za kutembelea vituo kwa ajili ya kukusanya taarifa.
Kikao kazi hicho kilishirikisha  Maafisa Utumishi wa Mikoa na Halmashauri, Waganga wakuu wa wilaya, Makatibu wa Afya wa Mikoa na Wilaya, Waratibu wa MTUHA wa Halmashauri na Wadau wa Maendeleo wa Mradi wa PS3.
Mfumo huo ni sehemu ya Mradi wa Uimarishaji wa Mifumo katika Sekta ya Umma – “Public Sector System Strengthening – (PS3) unaotekelezwa kwa ufadhili awatu wa Marekani kupitia USAID.
Tayari Halmashauri za mkoa wa lindi,Ruvuma na mtwara zimeshapatiwa mafunzo kwa kanda ya mtwara ikifuatiwa na mikoa ya Tanga na Pwani

mwisho
Na Abdulaziz Ahmeid

Comments