Wananchi
wa kijiji cha Katumba Azimio, kata ya Pito wameipongeza Halmashauri ya Manispaa
ya Sumbawanga kwa kuwajengea Zahanati inayotarajiwa kutoa huduma kwa kijiji
hicho na vijiji vya jirani vyenye jumla ya kaya 1,099.
![]() |
Zahanati ya Katumba Azimio |
Ujenzi
huo wa zahanati uliomalizika mwanzoni mwa mwezi Mei mwaka huu umegharimu shilingi
130,176,000 huku serikali kuu ikiwa imechangia shilingi 53,500,000, wananchi
nao wakiwa wamechangia shilingi 25,850,000 na manispaa ikiwa imechangia 50,826,000.
Mmoja
wa Wananchi wa kijiji cha katumba Azimio Herman Maufi amesifu kasi ya serikali
ya awamu ya tano katika kuhakikisha sekta ya afya inaimarika kuanzia ngazi ya
kijiji haji wilaya “Sisi tunamshukuru Mkurugenzi wetu wa Manispaa kwa kuona
umuhimu wa kutusogezea huduma hii karibu lakini Zaidi sifa hizi zimfikie rais
wetu jemedari Dkt. John Pombe magufuli kwakweli anapiga kazi.”
Nae
mwananchi mwingine wa kijiji cha jirani Tausi Juma amesema kuwa uwepo wa
zahanati hiyo unawasaidia kuepuka kwenda mjini kupata huduma hiyo na matokeo
yake watoto wao watapata huduma iliyokaribu nao na hatimae kuepuka gharama za
kwenda mbali kufuata huduma hiyo.
Comments
Post a Comment