Halmashauri
ya manispaa ya Sumbawanga kwa kushirikiana na Mfuko wa Mafao ya Kustaafu (GEPF)
wametumia shilingi bilioni 1.5 kupima viwanja na kuviwekea miundombinu katika
eneo la Nambogo mjini Sumbawanga kwa lengo la kuboresha makazi.
![]() |
Nambogo |
Afisa
Mipango Miji ardhi na maliasili wa manispaa ya Sumbawanga Thadeo Maganga amesema
kuwa mji wa Nambogo utakuwa ni mji wa mfano katika ukanda huu wa ziwa Tanganyika
na ziwa Rukwa katika kupunguza ujenzi holela kwenye miji inayoendelea kama
Sumbawanga.
“Kufanikiwa
kwa mradi huu utaijengea uwezo manispaa kupanga na kupima maeneo mengine na
kuzuia ujenzi holela na msongamano katikati ya mji pamoja na uuzwaji wa viwanja
hivi kuiongezea halmashauri mapato,” Alifafanua.
Jumla ya viwanja
2161 vimepimwa katika eneo hilo la Nambogo na Katumba Azimio kwa matumizi
mbalimbali ikiwemo makazi, makazi na biashara, shule, huduma za afya, maofisi,
kituo cha biashara (Shopping Mall), vituo vya mafuta, viwanja vya michezo na
maeneo ya kupumzikia.
Kati ya hivyo Viwanja vyenye ujazo wa juu (HD) 900, Viwanja vyenye ujazo wa kati (MD) 687, Viwanja vyenye ujazo wa chini (LD) 439, Viwanja vyenye ujazo wa chini uliozidi
(SLD) 126, Maeneo ya wazi (OS) 9.
viwango
vya matumizi ya viwanja.
Na
|
Aina
ya matumizi
|
Gharama
kwa kila mita ya mraba
|
1
|
Makazi
pekee (ujazo wa juu, kati na chini
|
2,700/=
|
2
|
Makazi
na biashara
|
3,000/=
|
3
|
Biashara
|
5,000/=
|
4
|
Huduma
za jamii
|
3,500/=
|
5
|
Ibada/
kuabudu
|
3,500/=
|
6
|
Hoteli,
vituo vya mafuta na maduka ya kuiwekezaji
|
5,000/=
|
Comments
Post a Comment