Sekondari ya Muhama kuboresha elimu ya sayansi


Mkurugenzi wa Manispaa ya Sumbawanga Hamid Njovu amesema kukamilika kwa maabara ya fizikia katika shule ya sekondari Muhama kutawaandaa wananfunzi wa shule hiyo kutekeleza sera ya viwanda na kuweza kujiari.

Maabara mpya ya Shule ya Sekondari Muhama

Amesema kuwa wanafunzi hawataweza kufanya vizuri katika masomo ya sayansi kama hawatawezeshwa kufanya masomo yao kwa vitendo hali itakayopelekea kutoa wanafunzi mahiri katika masomo hayo na kuongeza ufaulu.

“Maabara hii ya Sekondari ya Muhama ni kati ya maabara 9 zilizokamilika ujenzi wake katika Manipaa, tunaamini ukamilifu wake utaleta ushawishi kwa wanafunzi wa shule hii kupenda masomo ya sayansi pamoja na kurahisisha ufundishaji wa masomo hayo kwa waalimu,” Alisema.

Kwa upande wake Afisa elimu Sekondari Manispaa ya Sumbawanga Sylvester Mwenekitete amesema kuwa serikali ilijitahidi kutoa vifaa vya maabara lakini kwa ukamilifu wa majengo haya kutawezesha kuvihifadhi vifaa hivyo mahala salama.

Ujenzi huo wa maabara ya Fizikia umegharimu shilingi milioni 45, huku serikali huu ikiwa imetoa shilingi milioni 30, wananchi wakiwa wametoa shilingi milioni 13 na halmashauri kuchangia shilingi milioni 3.

Halmashauri katika kutekeleza agizo la ujenzi wa maabara tatu kwa kila shule ya sekondari, imefanikiwa kujenga vyumba vya maabara 51, ambapo vyumba 9 vya maabara vimekamilika na vyumba 42 viko katika hatua mbalimbali ya ukamilishaji.

Halmashauri ya manispaa ya Sumbawanga imetenga kiasi cha shilingi 234,656,000/= katika bajeti ya mwaka wa fedha 2017/18 kwa ajili ya ukamilishaji wa vyumba vya maabara katika shule za Sekondari 17.

Comments