Afisa Utamaduni aunda umoja wa wasanii Sumbawanga


Afisa Utamadunia wa Manispaa ya Sumbwanga Charles Kiheka amepania kuunda umoja wa wasanii wa maigizo katika manispaa ya Sumbawanga baada ya kutana na wasanii hao kwa lengo la kuwaelimisha namna ya kuweza kujisajili ili watambulike kisheria na kuisogeza Sanaa yao nje ya mipaka ya Mkoa nan chi kwa ujumla.

Amelifanya hilo baada ya kuona kuwa wasanii wengi wamekuwa wakilalamika kuwa kazi zao hazithaminiwi na wanunuzi na kukosa ushirikiano kutoka serikalini hivyo kupelekea maisha yao kuendelea kuwa duni licha ya kuipenda kazi wanayoifanya kwakuwa wanajipatia kipato kupitia kazi hiyo.

Afisa Utamaduni wa Manispaa ya Sumbawanga Charles Kiheka
“Wasanii mmekuwa katika makundi makundi, hamna ushirikiano katika kazi zenu, kila mtu ameonekana kujua kuliko mwengine, hampeani nafasi, hamshauriani kwa mwendo huu hatuwezi kufika na kama tutafanya kazi kwa ushirikiano tutakuwa mfano wa kuigwa n ahata halmashauri nyingine, Suluhisho pekee mimi nitasimamia uundwaji wa umoja wa wasanii katika Manispaa hii.” Kiheka alisem.

Katika kuhakikisha hilo linafanikiwa Ndugu Kiheka aliongeza kuwa ni wakati sasa umefika wa wasanii kusahau tofauti zao na kushikamana kwa pamoja ili kuhakikisha kuwa Sanaa ya Mkoa wa Rukwa inafahamika katika Nchi na dunia kwa ujumla.
Picha ya pamoja wasanii wa maigizo wa Sumbawanga

Nae kiongozi wa kikundi cha Sanaa cha Great Mind Association (GMA) Frank Dachi aliunga mkono hoja ya Afisa Utamaduni huyo na kusema kuwa kama wakongwe wa Sanaa wamepiti mengi na kati ya hayo hakuna faida waliyoiona kwa wao kutengana zaidi ya kuongezeka kwa uhasama baina yao na hatimae kuanza kugombea wasanii na kupelekea kazi zao kushindwa kuthaminika.

“Sisi wote ni watu wazima tumekuelewa Afisa, sisi tunaunga mkono yale yote uliyoyasema a tunakuhakikishia kwa usimamizi wako kama mwakilishi wa serikali kwenye hili tutafanikiwa, hapo mwanzo hatukuwa na kiongozi kama wewe ambaye aliwahi kutukutanisha pamoja kama hivi, tunashkuru sana,” Dachi alisem.

Kabla ya kumaliza mkutano huo Afisa Utamaduni aliweza kuwateua watu wanne ambao watakuwa viongozi wa muda wa umoja huo hadi hapo uchaguzi kamili utakapofanyika.

Comments