Afisa Utamaduni wa Manispaa ya Sumbawanga awaasa wasanii kujisajili BASATA


Afisa Utamaduni wa Manispaa ya Sumbawanga Kiheka Charles akimkabidhi cheti cha usajili wa kikundi cha Kwaya ya Mtakatifu Libori, Mwenyekiti wa Kikundi hicho ndugu, Zenobius Ndelwa katika ofisi ya Utamaduni, Manispaa ya Sumbawanga.
 Afisa Utamaduni wa Manispaa ya Sumbawanga, Kiheka Charles amewaasa wasanii wa Manispaa ya ya Sumbawanga kujisajili ili waweze kutambulika kisheria.

 Kiheka alihusia hayo alipokuwa akimkabidhi cheti cha usajili wa BASATA Mwenyekiti wa kikundi cha Kwaya ya Mtakatifu Libori chenye makazi yake katika kata ya Malangali ndugu Zenobius Ndelwa katika ofisi ya Utamaduni jengo la Manispaa ya Sumbawanga.

"Ni muhimu wasanii wote wajisajili ili wajijengee misingi ya kutambulika rasmi kiserikali na katika tasnia ya sanaa nchini. hii itawasaidia kuwajengea wigo mpana wa kufanya kazi ndani na nje ya nchi,"  Kiheka alisisitiza.

Afisa Utamaduni wa Manispaa ya Sumbawanga Kiheka Charles akimkabidhi cheti cha usajili wa kikundi cha Kwaya ya Mtakatifu Libori, Mwenyekiti wa Kikundi hicho ndugu, Zenobius Ndelwa katika ofisi ya Utamaduni, Manispaa ya Sumbawanga.














Comments