Watu 52 wakamatwa kwa kukaidi agizo la Rais kuhusu Usafi wa kila Mwisho wa Mwezi

Wananchi 52 wa Halmashauri ya Manispaa ya Sumbawanga watiwa nguvuni baada ya kukaidi agizo la Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. John Pombe Magufuli la kufanya Usafi kuanzia saa 1:00 hadi 4:00 asubuhi kila Jumamosi ya mwisho wa Mwezi.

Kati ya wananchi hao 52 ambao wengi ni wafanyabiashara ni 48 tu ndio waliofanikiwa kulipa faini ya shilingi 50,000/= kila mmoja na 2,400,000 zilikusanywa katika Mfuko wa mapato ya Manispaa, wananchi wane hawajalipa hivyo faini na taratibu za kuwafikisha mahakamani zinaendelea.

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Sumbawanga, Hamid Njovu
 “Zoezi la Kufanya Usafi ni la wananchi wote nchi nzima na hivyo ni wajibu wetu kutekeleza agizo la Rais wetu Dk. John Pombe Magufuli ili kuweza kuuweka mji wetu katika mazingira safi na salama wa Afya zetu” Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Sumbawanga Hamid Njovu aliyasema hayo wakati alipoongea na waandishi wa habari katika Ofisi za Manispaa.

“Wananchi hao walionekana kutojali agizo hilo na kuendelea na Biashara zao huku wananchi wengine wakiendelea na Usafi katika maeneo mbali mbali ya Mji wa Sumbawanga.” Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Sumbawanga alisema.

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Sumbawanga, Hamid Njovu akiongea na Waandishi wa Habari
Mkurugenzi wa Manispaa ya Sumbawanga Hamid Njovu alisisita na kutoa onyo kwa wale wote ambao watakaidi kwa jumamosi ya mwisho wa mwezi wa saba kuwa watazunguka maeneo mengi Zaidi ili kuona zoezi hili linatiliwa mkazo na wananchi wote wanashiriki kutekeleza agizo la Rais Dk. John Pombe Magufuli.

“Hatua kali za kisheria zikiambatana na faini na vifungo mbali mbali itakuwa inatekeleza bila ya uwoga wala huruma na zoezi hili la ukaguzi wa usafi wa maeneneo ya usafi na biashara itakuwa endelevu na wananchi wote waendelee kuchangia gharama za uzoaji wa taka kwa mujibu wa sheria ndogo za manispaa ya Sumbawanga.” Mkurugenzi Alimalizia.


Mkuu wa Idara ya Mazingira na Taka ngumu wa Halamashauri ya Manispaa ya Sumbawanga, Hamidu Masare

Comments