Mkurugenzi wa Manispaa atoa Shilingi Milioni 5 ujenzi wa ofisi ya kata Kizwite.

Ofisi ya Mkurugenzi wa halmashauri ya Manispaa ya Sumbawanga imetoa shilingi Milioni 5 katika kuunga mkono juhudi za wananchi wa Kata ya kizwite ili kupata ofisi mpya itakayoweza kutoa huduma kwa wakazi wa eneo hilo.

Ofisi hiyo ambayo imewekewa jiwe na Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Kamishna Mstaafu Zelote Stephen alipofanya ziara ya kutembelea miradi mbalimbali ya kimaendeleo inayofanywa na Manispaa ya Sumbawanga.
Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Sumbawanga Hamid Njovu akitoa ufafanuzi juu ya ofisi mpya ya kata ya Kizwite.
Katika kufanikisha ujenzi wa ofisi hiyo wananchi walijichangisha Shilingi milioni 2.97 na wahisani wengine walitoa shilingi 100,000.

Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Kamishna Mstaafu Zelote Stephen akimsalimia Afisa maendeleo ya jamii wa kata ya Kizwite Sepe, alipotembelea katika kata hiyo ili kuweka Jiwe la Msingi katika ofisi mpya ya kata hiyo

Mwenyekiti wa Mtaa wa Kizwite akisoma risala fupi ya ujenzi wa ofisi mpya ya kata ya Kizwite mbele ya Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Kamishna Mstaafu Zelote Stephen. (jengo lenyewe lipo nyuma ya waheshimiwa waliokaa)

(Waliosimama kuanzia kushoto)  Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Kamishna Mstaafu Zelote Stephen, akifuatiwa na Mkuu wa Wilaya ya Sumbawanga Mh. Mathew Sedoyyeka pamoja na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Sumbawanga Hamid Njovu wakimsikiliza kwa makini mwananchi David Msongole aliyeuliza juu ya swala la elimu bure na kutaka majibu.

Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Kamishna Mstaafu Zelote Stephenaliweza kumjibu vizuri juu ya taratibu zinazotakiwa kufuata katika kuendesha hilo suala la elimu bure. ikiwemo wananchi kuweza kutoa wazo la kuchangia mambo ya kimaendeleo katika shule za watoto wao bila ya upata ushawishi kutoka kwa watumishi wa serikali.

Comments