Asilimia 26 inahitajika kuondoa upungufu wa madawati Katika Shule za Manispaa ya Sumbawanga.

Katika kutekeleza agizo la Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. John Pombe Magufuli la kutotaka kusikia mwanafunzi anakaa chini ifikapo tarehe 30, June 2016, Halmashauri ya Manispaa ya Sumbawanga imetumia shilingi Milioni 50.8 kutengenezea madawati ili kuona Zoezi hilo linafanikiwa.

Pamoja na jitihada hizo Halmashauri ya Manispaa ya Sumbawanga bado inakabiliwa na upungufu wa madawati 5,142 kwa shule za Sekondari na Msingi huku asilimia 99 ya uhitaji huo ni katika shule za Msingi za Manispaa hiyo.
Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa wa Sumbawanga Hamid Njovu (aliyevaa miwani) akimuelekeza Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Kamishna Mstaafu Zelote Stephen (hayupo pichani) kwa wakuu wa Idara wa Manispaa ya Sumbawanga, akiwa na Mstahiki Meya wa Manispaa ya Sumbawanga Mh. Justin Malisawe (aliyevaa Shati la kitenge)
Halmashauri ya Manispaa ya Sumbawanga ina jumla ya shule za Msingi za seriakali 55 na Sekondari 17, ambapo tangu mwaka huu uanze madawati 5,411 maptayari yameshatengenezwa na 1,367 yamekarabatiwa.

Mchumi wa Manispaa wa Sumbawanga Saad Mtambule alisema kuwa changamoto kubwa ni ukosefu wa fedha katika kufanikisha hili na Mvua nyingi zilizonyesha mwezi Februari hadi Aprili zilisababisha mbao kutokauka mapema.

Lakini pamoja na Hayo Ng. Mtambule alisema “Pamoja na Changamoto hizo kuna Jitihada kadhaa ambazo tunazifanya ili kukamilisha zoezi ikiwemo kupasua mbao katika msitu uliyopo kwenye baabara ya kwenda Kasanga kwa kibali cha TANROAD na pia kuendelea kupasua mbao katika miti iliyopo mashuleni”

Pia Mchumi wa Manispaa, Mtambule alongeza kuwa juhudi za kuwashawishi wadau wa maendeleo bado zinaendelea na pia kutenga bajeti katika mapato ya ndani ya manispaa ili kuweza ufanikisha Zoezi hilo.

Milioni 308.5 bado zinahitajika ili kufuta upungufu wa madawati katika Halmashauri ya Manispaa ya Sumbawanga.

Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Kamishna Mstaafu Zelote Stephen(aliyevaa miwani) akiongozana na viongozi wenziwe kuangalia Madawati.
Hivyo kama wewe ni Mdau wa maendeleo unaeishi Katika Masipaa ya Sumbawanga usisite kuchangia ili wananfunzi ambao ndio Taifa la Kesho wawe na Mazingira mazuri ya kupata Elimu. 

Comments