Madiwani wa Sumbawanga wapewa mafunzo ya usimamizi wa fedha.



Madiwani wa Halmashauri ya Manispaa ya Sumbawanga wapatiwa mafunzo ya usimamizi na udhibiti wa fedha ili kuwapa uwezo wa kusimamia vyanzo mbalimbali vitakavyoongeza mapato katika manispaa hiyo.

Mafunzo hayo yalifanyika katika ukumbi wa manispaa ya Sumbawanga na kuendeshwa na katibu tawala wa serikali za mitaa kutoka ofisi ya mkuu wa mkoa wa Rukwa Ndugu Albinus Mgonya.

Katibu Tawala serikali za mitaa ndg. Albinus Mgonya akiendelea na mafunzo,
Ndugu Mgonya alisema kuwa mafunzo hayo yamelenga kuwaongezea ufahamu waheshimiwa madiwani ili kuweza kusimamia vyanzo vya mapato kwa uangalifu mkubwa na kuwa, mafunzo hayo yametolewa kwa madiwani walio katika halmashauri zilizo katika mikoa kumi nchini. 

Vigezo vilivyotumika kuchaguliwa kwa mikoa hiyo  ni pamoja na halmashauri zake kupata hati zisizorisha, chafu au mbaya, pia halmashauri kutofanya vizuri katika makusanyo yake ya ndani pamoja na mikoa yenye halamashauri mpya.

Wakati mafunzo hayo yakiendelea baadhi ya madiwani waliuliza maswali mbali mbali li kuweza kupatiwa majibu na kuweza kujua nafasi zao na kutambua majukumu yao kudhibiti mapato ya ndani ya halmashauri. 

Mh. Vitalis Ulaya, diwani wa kata ya Msua alitaka kujua utoaji wa taarifa za fedha ukoje, swali ambalo lilijibiwa na Mkurugenzi wa Manispaa ya Sumbawanga ndugu. Hamid Njovu kwa kueleza kuwa kamati ya fedha hukutana kila mwezi kupokea taarifa ya mapato na matumizi na hatimae kamati hiyo hutoa ushauri kwa wataalamu wa manispaa inapoona inafaa. 


Mkurugenzi wa Manispaa ya Sumbawanga ndg. Hamid Njovu akijibu swali.

Kabla ya kumaliza mafunzo hayo ndugu Mgonya aliwasihi waheshimiwa madiwani kuwahamasisha wananchi wanaowaongoza katika kata zao juu ya kuchangia katika miradi mbalimbali ya kuendeleza halmashauri kupitia katika kamati zao za maendeleo.

Waheshimiwa Madiwani wa Manispaa ya Sumbawanga wakisikiliza mafunzo.
 “wananchi wanapokuwa wanachangia ile asilimia 2 ya mradi huwafanya wanachi kuuona ule mradi kuwa ni wa kwao na kuweza kuulinda kwa nguvu zote na kuuonea uchungu” Mgonya alisisitiza.

Comments