Kidato cha Sita wamaliza mitihani salama - Sumbawanga



Mitihani ya kumaliza kidato cha sita mwaka 2016 yafanyika kwa Amani na kwa utulivu katika halmashauri ya Manispaa ya Sumbawanga. Mitihani ilianza siku ya Jumatatu tarehe 2/5/2016 na kumalizika tarehe 11/5/2016. Jumla ya vituo ni 6 vyenye watahiniwa 612 waliosajiliwa, wakiwemo watahiniwa 450 wa shule na 162 wa kujitegemea.

Katika kufafanua yaliyojitokeza afisa elimu sekondari Sylvester Mwenekitete alisema “Kwa jumla hali ya mahudhurio ya watahiniwa ilikuwa nzuri. Hata hivyo, katika kituo cha Msakila mtihani wa Advance Mathematics ilipelekwa lakini watahiniwa hawakuwepo hivyo mitihani hii ilikabidhiwa kwa kamati ya uendeshaji wa mitihani mkoa”

Miongoni mwa shule zilizofanya mtihani huo ni Shule ya sekondari St. Maurus, Shule ya sekondari Kizwite, Shule ya sekondari Kantalamba, Shule ya sekondari Msakila, Shule ya sekondari Sumbawanga na Shule ya sekondari Aggrey Chanji.

Walimu wa Shule ya Sekondari Sumabwanga

Hakukutokea na sifa yoyote ya wizi wa mitihani wala udanganyifu wa aina yoyote. Hii ilitokana na umahiri wa ulinzi wa mitihani hiyo uliotolewa na jeshi letu la askari polisi wa wilaya likishirikiana na kamati ya uendeshaji wa mitihani ya mkoa.

“ Nawatakia kila la heri katika maisha yao ya baada ya shule ya Sekondari”  Mwalimu mkuu wa shule ya sekondari ya Kizwite bwanaLazaro Mwandenene alitoa neno lake la mwisho kwa wanafunzi wote waliomaliza salama mitihani ya kidato cha sita.

Comments