Sekta ya Afya Sumbawanga bado inajikongoja

Kama ilivyokuwa kwa mpango wa BIG RESULT NOW (BRN) uliolenga kuboresha elimu nchini, zoezi hili limegeukia upande wa sekta ya afya ili kuboresha utoaji huduma za kiafya kuanzia ngazi ya zahanati kwenye kata hadi hospitali za wilaya.

Zoezi lilifanywa na timu ya utafiti kutoka wizara ya Afya,maendeleo ya jamii,jinsia, wazee na watoto iliyoongozwa na Dokta Zuwena Bakari ikishirikiana na wahudumu wa afya wa Manispaa ya Sumbawanga kupitia vituo vya afya 39 vya Mansipaa vikiwemo vya serikali, mashirika ya dini na watu binafsi ili kujua uwezo wa vituo hivyo kutoa huduma za afya.

Timu hii ya utafiti iliyoundwa na watu 10 ilitumia siku 10 kupitia vituo vyote vya afya na iliangalia mambo manne ili kuweza kutoa hadhi ya uwezo wa kituo, mambo hayo yakiwemo idadi ya watumishi, utoaji wa tiba,utendaji kazi wa watumishi pamoja na huduma wa afya ya uzazi kwa kina mama wajawazito na watoto chini ya umri wa miaka mitano.

Hadhi hizo zilitolewa kwa mfumo wa Nyota huku nyota tano ikimaanisha vizuri sana na nyota moja bado sana na ambazo hazina nyota ikiwa na maana hazifai kutoa huduma mpaka hapo mambo muhimu yatakapofanyiwa kazi.

Ni 72% ya vituo hivyo ndivyo vilivyopata nyota 1 na 2 na 28% havikupata nyota hata moja, jambo ambalo linahitaji kutazamwa kwa jicho la kipekee maana taifa bila ya watu kuwa na afya nzuri haliwezi kujengeka.
Dk.Zuwna bakari akitoa ufafanuzi wa ripoti


“asilimia kubwa ya zahanati hazina vyumba maalum vya kumchunguza mgonjwa kwa siri na pia nyingi hazina magodoro na kupelekea wazazi wanaotaka kujifungua kulalia misengela(mikeka) hali hii inasikitisha” Dokta Zuwena alisema.

Pia Dk. Zuwena aliongeza kuwa 90% ya vituo hivyo havina umeme wa uhakika na kupelekea watu kutumia vibatari na mishumaa jambo ambalo ni hatari kwani inaweza kusababisha matatizo makubwa Zaidi.


Mbali na hayo Dk. Zuwena  alisikitishwa na ukosefu wa maji wa asilimia 51 katika vituo walivyovitembelea na kuonya kuwa kama kama magonjwa ya mlipuko kama kipindupindu kinatokea uzuiwaji wake utakuwa mgumu maana hata manesi watashindwa kutoa huduma ipasavyo.

Comments