Manispaa ya Sumbawanga yaibamiza NMB 3 - 1

Waendesha Halmashauri ya Manispaa ya Sumbawanga wamewatandika bila ya huruma wahesabu fedha wa Benki ya NMB tawi la Sumbawanga magoli 3 -1 katika mchezo wa kirafiki uliochezwa uwanja wa Nelson Mandela uliopo mjini Sumbawanga.

Magoli yote matatu ya Manispaa ya Sumbawanga yalipatikana Kipindi cha pili cha mchezo huo baada ya wachezaji hao kupata maelekezo ya Kiufundi kutoka kwa kocha anaetambulika kimataifa Adam Evarist.

Goli moja la wahesabu fedha hao lilipatikana kwa penati baada ya Mchezaji wa Manispaa ya Sumbawanga kuunawa mpira.

Hapo awali kulikuwa na taarifa ya kuwepo kwa michezo miwili yaani mchezo wa mpira wa miguu kwa wanaume na mpira wa netiboli kwa wanawake lakini hadi mchezo wa mpira wa miguu kwa wanaume unakwisha wahesabu fedha hao wa kike hawakuonekana uwanjani jambo ambalo liliwahuzunisha waendesha Manispaa wa Kike, kwani walipania mchezo huo.

Mmoja wa viongozi wa wahesbu fedha alisema kwa uchungu kuwa atafanya juu chini mechi irudiwe ili waweze kuhamisha kilio katika Ofisi ya Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Sumbawanga.

Picha Zote na Irene Chale 
Picha ya Pamoja. FAIR PLAY
Kikosi cha Manispaa ya Sumbawanga 

Mashabiki na wafanyakazi wa Halmashauri ya Manispaa ya Sumbwanga 

Mpira ukiendelea
Timu ya Halmashauri ya Manispaa ya Sumbawanga wakati wa Mapumziko.
Timu ya Netiboli Timu ya Halmashauri ya Manispaa ya Sumbawanga wakifanya Mazoezi baada ya timu ya benki ya NMB kuingia Mitini.
Goli la Penati la Benki ya NMB

Goli la kwanza lilipofungwa 

Mpira ukiendelea

Mpira ukiendelea

Benchi la Ufundi la timu ya Benki ya NMB tawi la Sumbawanga

Mpira ukiendelea

Mpira ukiendelea

Mpira ukiendelea

Kocha Maarufu wa Timu ya manispaa ya Sumbawanaga Adam Evarist akiangalia mpira unavyoendelea. 

Mpira ukiendelea

Mpira ukiendelea

Mfungaji wa Magoli mawili ya Timu ya Manispaa ya Sumbawanga Mahmud Mohamed

Kocha Maarufu wa Timu ya manispaa ya Sumbawanaga Adam Evarist Akimpa hongera mchezaji wake aliyefunga magoli mawili katika Mchezo wa kirafiki kati ya Manispaa ya Sumbawanga na Benki ya NMB tawi la Sumbawanga

Mpira ukiendelea

Dereva Maarufu wa Manispaa ya Sumbawanga Mjomba Iddi

Mpira ukiendelea

Washabiki wa NMB wakiwa wamekata tamaa

Mpira ukiendelea


picha ya pamoja 

Comments