Tatizo la Madawati Sumbawanga

Katika kutekeleza agizo la Rais John Pombe Magufuli la kuhakikisha kuwa mpaka mwezi wa sita mwaka 2016 hakutakiwi kuonekana mwanafunzi anakaa chini kwa kukosa dawati, Halmashauri ya Manispaa ya Sumbawanga imedhamiria kushirikiana na wadau wa elimu ili kuhakikisha kuwa watoto wetu wanapata elimu bora kwa kukaa katika madawati katika     mazingira bora.

Moja ya kuhakikisha lengo hili  kwani hatuwezi kuwa na elimu bora wakati watoto wetu wanakaa chini, wanakaa kwa  kubanana katika madarasa na kusoma katika   madarasa yaliyo na vumbi.

Halmashauri ya Manispaa ya Sumbawanga ina Shule 72 za serikali ikiwa 55 za Msingi na 17 za sekondari. Hadi sasa Manispaa ya Sumbawanga ina wanafunzi 56,457 kwa shule za msingi ikiwa wavulana 27,039 na wasichana 29,418.

Mfumo wa uendeshaji wa Elimu unaagiza uwiano wa dawati 1 kwa wanafunzi 3 hivyo kutokana na idadai ya wanafunzi 56,457 Halmashauri inahitaji kuwa na madawati 18819 ila hadi sasa Halmashauri ina madawati 9484 na kufanya upungufu wa madawati 9385.

Halmashauri imetoa pesa kiasi cha sh. 10,000,000/= kwa ajili ya upasuaji mbao katika Maeneo Mbalimbali yaliyopandwa miti, maeneo hayo ni kama vile katika Shule zetu za Msingi na Sekondari.  Kupitia Miti hiyo Halamshauri inatarajia kuvuna mbao zenye  kipimo cha 1” x 8” x 10 kiasi cha mbao 3000 hadi 3500.

Halmashauri imeagiza square pipe 1000 zenye thamani ya sh. 12,000,000/= ambazo zinaweza kutengeneza fremu za madawati 500.

Halmashauri imeagiza walimu wakuu kutumia 30% za fedha za capitation za uendeshaji wa shule kwa ajili ya kukarabati madawati mabovu ili kupunguza uhaba huo. Na kupitia Fedha hizo Halmashauri inatarajia kutengeneza Madawati 894.

Mfumo wa uendeshaji wa shule za Sekondari unahitaji kuwepo kwa meza na kiti cha mwanafunzi I kwa ajili ya Wanafunzi wa shule za Sekondari. Sekondari za Manispaa zilikuwa zinahitaji Meza 4211 na viti 4211 Halmashauri ina upungufu wa meza 1476 na viti 957.

Hivyo ni jukumu letu kama wadau kuinua kiwango cha elimu katika Manispaa yetu ya Sumbawanga kwa kuhakikisha kuwa tunakuwa na mazingira bora ya kufundishia na kusomea watoto wetu.

Kwa maelezo Zaidi piga simu kwa Mkurugenzi wa Manispaa 0624 777666

Au tuma kwenye Akaunti ya NMB 62110001801



Comments